Thursday, August 14, 2008

Wafanyakazi wa ndani

Wafanyakazi wa ndani ni watu muhimu sana katika familia zetu. Hushughulika na kupika, kufua, na unakuta ndie anabaki na mtoto ikiwa baba na mama wanafanyakazi. Ni vizuri tukawaheshimu na kuwafanya kuwa ni sehemu ya familia yetu.

Familia zinatofautiana, zipo familia zinaaowaona wafanyakazi wa ndani kama watumishi. Kwa upande wangu ninalaani kitendo hicho. Tuwape haki. Si kuwatumikisha bila kuwapa ajira yao. Walipwe kulingana na makubaliano walioekeana baina yao. Wakati mwingine wafanyakazi wa ndani huwa ndio wa mwisho kula na hata kulala. Wao ni binadamu kama wengine huwa wanachoka na wanahitaji muda wa kupumzika.

Swali: Je hayo yanatokea kwenye familia zetu.
Ni nini kifanyike?

No comments: