Thursday, September 18, 2008

MISITU NI DAHABU

Misitu ni muhimu sana kwa maisha ya binadamu. Hutupatia dawa, kuni, mkaa na mbao. Misitu pia huvuta mvua, hutoa kivuli kwa ajili ya kupumzika pia misitu ni makazi ya wanyama. Faida hizi zote huweza kutoweka kwa muda mfupi iwapo matumizi hayatakuwa endelevu.

Uvunaji wa mazao ya misitu usioangalia na kukifikiria kizazi kijacho, huo in uharamia wa misitu. Uharibifu wa misitu umjitokeza sehemu mbalimbali hapa nchini. Mfano dhahiri ni misitu ya RUVU KUSINI. Misitu hiyo hukatwa kwa matumizi ya mkaa, kuni na mbao. Msitu huu umekuwa kama hauna mwenyewe. Chakushangaza ni kwamba msitu huu ni wa hifadhi ya Taifa.

Wananchi wanoishi karibu na msitu huu wanasema kwamba hawaoni umuhimu wa msitu huu kwao, kwani hawaoni faida nyingine tofauti na nilizozieleza hapo juu. Siku za nyuma walikuwa wakiulinda na kukamata maharamia pamoja na mazao waliyovuna msituni. Mazao hayo yalikuwa kama mbao, magogo ya kujengea, mkaa na kuni. Mazao hayo yalichukuliwa na serikali kuu pasipo kubakiza chochote katika kijiji. Mali iliyokamatwa iliuzwa kwa fedha nyingi sana lakini hakuna chochote kilichorejeshwa kwa wananchi au kijijini. Kwa sababu hiyo wananchi wakaamua kuacha watu wajivunie msitu kama wao.

Tatizo la yote hayo ni kutowashirikisha wananchi katika ulinzi wa misitu. Wananchi washirikishwe kwenye ulinzi wa misitu na faida zitokananzo na mazao ya misitu zigawanye kwa makubaliano ya wananchi. Sheria zitungwe au zitumike kuwaadhibu wanatumia misitu kinyume na taratibu. Pia wananchi waleimishwe umuhimu wa misitu na matatizo ya kutokuwa na misitu.

Thursday, September 11, 2008

UNYANYAPAA NA VIRUS VYA UKIMWI

Nilisikiliza kipindi cha Femina Talkshow cha wiki hii kwa masikitiko makubwa sana. Kuna dada mmoja mlemavu alipata ukimwi na kutelekezwa na familia yake. Mwanadada huyo aliamua kueleza wazi kuwa ni muadhirika akitegemea kupata msaada kutoka kwa familia yake. Chakushangaza ni kwamba alinyanyapaliwa na kutengwa na familia yake. Kwa sasa analelewa na mtu aliye wa familia yake. Ni ndugu wa kutoka kijiji kimoja. Mambo kama hayo yapo kwenye familia nyingi. Ndio maana tulio wengi tunaogopa kujitangaza. Kwani kujitangaza ni kunyanyapaliwa na jamii na pia kutengwa. Huyu mlemavu alijitoa mhanga na kujitangaza. Alikuwa na ujumbe mzito kwa wa-Tanzania. Kwani tulio wengi tunadhani walemavu hawana ukimwi? Dunia imebadilika. Hakuna mlemavu, watoto wa shule wala nani. Wote wanao. All are vulnerable to HIV/AIDS.

Ni wajibu wetu kama jamii kuwahudumia waadhirika wa ugonjwa huu kwa hali na mali. Kwani wote ni watarajiwa wa ugonjwa huo. Nilisoma jana kwenye jamii forums kwamba kuna mtoto alikuja papai na kupata HIV. Uchunguzi ulipofanyika uligundua kwamba aliyemuuzia mtoto huo papai alikuwa na jeraha liliokuwa linatoa damu. Kwa hali hiyo mtoto alipata ukimwi kwa nia hiyo. No one is safe against this killer disease.
Ninatoa pongezi kwa kipindi cha Femina Talk Show hiki kwani kinatoa mambo muhimu yanayozikumba jamii zetu. Kwa hiyo tujifunze kupitia kipindi hiki.

Monday, September 8, 2008

Bei ya Nyama Jiji Dar Sasa Inatisha

Maisha ya mwananchi wa kima cha chini yanakuwa magumu siku hadi siku. Wiki iliyopita bei ya nyama ilikuwa ni shilingi 3,200 kwa kilo kwa fedha ya ki-Tanzania. Juzi nilinunua nyama hiyo hiyo kwa shilingi 3,400 kwa kilo. Cha kushangaza ni kwamba leo asubuhi nimenunua nyama kwa shilingi 3,600 kwa kilo moja. Je tutafika?
Ninachojiuliza ni kwamba wakati wa mfungo Mtukufu wa Ramadhani nyama inatumika kwa wingi sana au tatizo lipo wapi? Nikiangalia sioni sababu ya kufanya nyama ambayo ni kitoweo muhimu kwa wananchi kupanda hasa wakati wa sikukuu kubwa kama hii ya Mfungo, X-Mass na Pasaka. Ninadhani kuna haja ya kufanya juhudi za ziada ili kutuokoa sisi wa-Tanzania

Saturday, September 6, 2008

Asilimia 40 ya bidhaa nchini ni feki

Je tutafika? Leo nimesikia kwenye vyombo vya habari kuwa asilimia arobaini ya bidhaa zinazouzwa hapa nchini ni feki, zisikuwa sahihi kwa matumizi ya binadamu. Hii hali imenishtua sana. Kwani ni vigumu watu au watanzania tulio wengi kugundua au kujua kitu ambacho ni FAKE au GENUINE. Zinahitajika juhudi za ziada kuwaokoa wa-Tanzania. Kinyume na hapo tutalipoteza taifa hili.Cha kujiuliza, hizo bidhaa feki hadi kufikia asilimia arobaini zinaingiaje nchini? TRA wananfanya nini? TBS wanafanya nini? Wafanyakazi mipakani, viwanja vya ndege na bandarini wanafanya kazi gani? Hayo ni maswali ambayo sina majibu la haraka. Je nini kifanyike. Nchi inanuka rushwa. Maisha ya wananchi yapo hatarini.
This ad zapped.

Monday, September 1, 2008

Gardens along Morogoro Road

One of the income generating acitivity in the city of Dar es salaam is selling seedlings and flowers. When moving along Morogoro road you will see a lot of people selling seedlings/plants of different kind. At the same time you will see different people parking their car along the road buying seedlings and flowers.Last week I interviewed one owner of those gardens and comment that,this business is not always giving them money. Because the customer buy their products at great quantity during rain seasons compared to dry season, as you know Dar es Salaam is not secured for water supply .So during rain time the soil is wet to support the plants thats why many people would like to buy seedlings.The problem gardeners are facing is the small capital they have. They also lack education on how to improve their business as well as it is difficult to predict the market situation. Somedays they failed even to sell one seedlings. My concern here is that how those gardeners can be assisted