Friday, February 29, 2008

CURRICULUM VITAE (CV)

Personal Particulars
Full Name: Emmanuel Patroba Mhache
Date of Birth: December 24th 1970
Place of Birth: Moshi ®, Kilmanjaro
Marital Status: Married with one wife and one child
Sex: Male
Nationality: Tanzanian
Contacts: P.O. Box 78402, Dar es Salaam,
Tanzania.
E-mail: ngorora@yahoo.com, ngororamhache@gmail.com
Mobile: 0754 383 416
Academic Qualifications
University Education
:
October 2002 to September 2004
Master of Arts in Geography and Environmental Management (M.A. GEM) obtained from the University of Dar es Salaam.
September 1995 to June 1998
Bachelor of Arts (B.A) Degree; First Class Degree Honours in Land Use Planning and Environmental Studies, from the University of Dar es Salaam.
Secondary Education:
1991 to 1993 and1987 to 1990
Advanced Level Certificate of Secondary Education studied in Tanga, Galanos Secondary School and Ordinary Level Certificate of Secondary Education in Kilimanjaro, Natiro Secondary School respectively.
Research Experience
July 23rd 2003 to September 19th 2003
As a Researcher: Impacts of Tree Planting on the Livelihood of Communities in Unguja, Zanzibar.
As a Research Assistant: Interaction between Forest Plantation and Community and its Impact on Biodiversity in Zanzibar, Tanzania. This research was done in collaboration with the Lecturers and Students of the University of Dare es Salaam and University of Turku, Finland.
Training, Seminars, Workshops and Conferences Attended
March 6th 2000 to April 6th 2000: Attended and completed PRIDE Credit Officers Induction Training courses and awarded Certificate upon successful completion of the training conducted in Nairobi, Kenya.
December 8th 2004 to December 9th 2004
Attended and participated in a seminar held in the University of Turku, Finland. In that seminar I presented a paper with heading: Pete Village, Life and Environment. This village is located Southern Zanzibar.
December 16th 2004 to December 17th 2004
Participated in a Seminar workshop organized by Organization for Social Science Research in Eastern and Southern Africa (OSSREA). In this two-day seminar I presented paper titled, “Impacts of Tree Planting on the Livelihood of Communities in Unguja, Zanzibar”.
1st July 2007 Attended seminar on writing of study material and course outline for a proposed B.Sc. Degree Programme in Environment Studies held in the Conference room of Giraffe Jangwani Hotel Beach and 22nd August to 24th August 2007 I attended and successfully completed seminar on Project Management Skills and Techniques organized by the Open University of Tanzania held at the Morogoro Hotel – Morogoro, Tanzania.
28th August 2007: Gender sensitization seminar for academic staff held at the Open University of Tanzania. It was a one day seminar.
Other Qualifications:
Computer knowledge especially in Microsoft Word, Microsoft Power Point as well as data entry and analysis using Microsoft Excel and Statistical Package for Social Sciences (SPSS). I am familiar with remote sensing and GIS because I studied these causes.
Employment Records:
April 17th 2000 to July 30th 2003 and 17th March, 2005 to 30th September, 2006: Working with PRIDE Tanzania Limited, as a Credit Officer and Micro Finance Information Officer (MIS Officer)
August 2005 to 1st October, 2006
Working with The Open University of Tanzania as Part-Time Lecturer in Geography, while 2nd October, 2006 to date: Working with The Open University of Tanzania as an Assistant Lecturer in Geography.
Publications:
Mhache E. P. 2005. Impacts of Tree Planting on the Livelihood of Communities in Unguja, Zanzibar. Turku University Department of Geography. Publication B. Nr 1.
Mhache E. P. 2005. Muingiliano Kati ya Mashamba ya Misitu ya Serikali ya Kupandwa na ya Jamii na Athari Zake Katika Bioanuwai Zanzibar, Tanzania. Turku University Department of Geography. Publication B. Nr 4.
Mhache E. P. 2007. Deforestation as an Obstacle to Sustainable Development: The role of Higher Learning Institutions in Sustainable Responses. Published paper in Huria Journal Vol. 2 /No. 1 of 2007.
Referees:
1. Dr. Elias Songoyi,
The Open University of Tanzania (OUT),
P.O. Box 23409,
Phone No. 0784 773 466
E-mail: eliasnandi@yahoo.co.uk
Dar es Salaam.

2. Dr. Jacqueline Bundala,
The Open University of Tanzania (OUT),
Geography Department,
P.O. Box 23409,
Phone No. 0714 256 501,
E-mail: mwibu@yahoo.co.uk
Dar es Salaam.

Wednesday, February 13, 2008

Valentine Day

What is valentine day?

To some people, call it as a day when all lovers meet and enjoy together.

I wish all bloggers good, cheerfull and prosperous day.

God bless you all.

Tuesday, February 12, 2008

Waliopita mchujo ni hawa

Baraza la Mawaziri jipya lililotangazwa jana na Rais Jakaya Kikwete lina jumla ya mawaziri na manaibu 47, wakiwemo wanawake 12, tofauti na lililovunjwa ambalo lilikuwa na idadi ya mawaziri na manaibu 60. Kati ya Mawaziri na Manaibu 60 wa Baraza lililopita 15 walikuwa wanawake na katika Baraza jipya wanawake wanne wameenguliwa na mmoja alifariki.
Aidha, jumla ya mawaziri tisa na manaibu wanane waliokuwa katika baraza lililopita wameenguliwa katika baraza la sasa. Katika Baraza hilo jipya, mawaziri wako 26 na manaibu 21 ambapo sita kati yao hawakuwepo kwenye baraza lililopita. Sura mpya katika baraza la sasa ni pamoja na Bi. Lucy Nkya, Dk. James Wanyancha, Hamisi Kagasheki, Adam Malima, Ezekiel Maige na George Mkuchika.
Halikadhalika, baadhi ya waliokuwa manaibu waziri, sasa wamepewa wizara kamili. Hawa pamoja na wizara zao za zamani kwenye mabano ni William Ngeleja (Wizara ya Nishati na Madini), Mustapha Mkullo (Fedha), Shamsa Mwangunga (Maji), Lawrence Masha (Mambo ya Ndani), Mathias Chikawe (Katiba na Sehria na Diodorus Kamala (Ushirikiano wa Afrika Mashariki).
Baraza zima la sasa ni kama ifuatavyo: Waziri wa Nchi (Utawala Bora) ni Bi. Sophia Simba wakati Waziri wa Nchi (Menejimenti ya Utumishi wa Umma) ni Bi. Hawa Ghasia. Wizara nyingine ambazo ziko chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais ni ile ya Muungano ambayo Waziri wake ni Bw. Mohammed Seif Khatib na ya Mazingira inayoongozwa na Dk. Batilda Buriani. Kwa upande wa Wizara zilizo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge inaongozwa na Bw. Philip Marmo wakati ile ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Waziri wake ni Bw. Steven Wasira na Naibu ni Bi. Celina Kombani. Wizara ya Mipango na Fedha Waziri ni Bw. Mustapha Mkulo na manaibu wake ni Bw. Jeremiah Sumari na Bw. Omar Yusuph Mzee. Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii imebakia na Mawaziri wake wale wale, Profesa David Mwakyusa na Naibu wake, Dk. Aisha Kigoda wakati Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi sasa Waziri wake John Chiligati. Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi itakuwa chini ya Waziri Profesa Jamanne Maghembe na Manaibu wake Bi. Gaudentia Kabaka na Bi. Mwantumu Mahiza.
Dk. Shukuru Kawambwa ni Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia na Naibu wake ni Dk. Maua Daftari wakati Wizara ya Miundombinu itabaki kama ilivyokuwa, yaani Waziri Andrew Chenge na Naibu Dk. Makongoro Mahanga. Kwa upande wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Waziri wake sasa ni Kapteni George Mkuchika na Naibu wake ni Bw. Joel Bendera wakati Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana Waziri atakuwa Profesa Juma Kapuya na Naibu Bw. Hezekiah Chibulunje. Wizara ya Maji na Umwagiliaji itaongozwa na Profesa Mark Mwandosya na Naibu ni Bw. Christopher Chizza wakati Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika Waziri ni Profesa Peter Msola na Naibu ni Dk. Mathayo David. Aidha Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto itakuwa chini ya Waziri Bi. Margaret Sitta na Naibu Dk. Lucy Nkya wakati ile ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Waziri ni Bw. John Magufuli akisaidiwa na Dk. James Wanyancha. Wizara ya Maliasili na Utalii itaongozwa na Bi. Shamsha Mwangunga na Naibu wake ni Bw. Ezekiel Maiga. Wizara ya Mambo ya Ndani waziri wake sasa ni Bw. Lawrence Masha na Naibu wake ni Balozi Khamis Kagasheki wakati Waziri Bernard Membe na Naibu wake Balozi Seif Idd wanaendelea kuongoza Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Wizara ya Nishati na Madini itakuwa chini ya Waziri William Ngeleja na Naibu ni Bw. Adam Malima. Wizara ya Katiba na Sheria itaongozwa Waziri Mathias Chikawe, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa itaongozwa na Dk. Hussein Mwinyi na kusaidiwa na Dk. Emmanuel Nchimbi. Kwa upande wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Diodorus Kamala anakuwa Waziri na Naibu wake ni Bw. Mohamed Abood Mohamed wakati Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko itaongozwa na Waziri Dk. Mary Nagu na Naibu wake akiwa Dk. Cyril Chami. Aidha Mawaziri walioenguliwa na wizara zao kwenye mabano ni Bi. Zakhia Meghji (Fedha), Dk. Harith Mwapachu (Usalama wa Raia), Bw. Bazil Mramba (Viwanda, Biashara na Masoko). Wengine ni Bw. Joseph Mungai (Mambo ya Ndani), Dk. Juma Ngasongwa (Mipango, Uchumi na Uwezeshaji), Bw. Kingunge Ngombale Mwiru (Siasa na Mahusiano ya Jamii) na Bw. Anthony Diallo (Maendeleo ya Mifugo). Mawaziri wengine ni Dk. Ibrahim Msabaha (Ushirikiano wa Afrika Mashariki) na Bw. Nazir Karamagi (Nishati na Madini). Manaibu Mawaziri walioenguliwa na wizara walizokuwa wakiongoza kwenye mabano ni Bw. Abdisalim Khatib (Fedha), Bi. Zabein Mhita (Maliasili na Utalii), Bi. Ritha Mlaki (Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi), Bw. Luka Siyame (Ofisi ya Waziri Mkuu), Bw. Ludovick Mwananzila (Elimu na Maunzo ya Ufundi). Wengine ni Bw. Daniel Nsanzugwanko (Habari, Utamaduni na Michezo), Bw. Gaudence Kayombo (Mipango, Uchumi na Uwezeshaji) na Bw. Charles Mlingwa (Mifugo). Wakati huo huo, Rais Jakaya Kikwete amesema katika kipindi cha miaka miwili ya serikali ya awamu ya nne walikuwa wakitazama muundo wa serikali na hivyo sasa amelazimika kupunguza ukubwa wa serikali kulingana na mahitaji ya wakati uliopo. Aliyasema hayo wakati akitangaza Baraza jipya la Mawaziri mjini Dodoma jana. Alisema ukubwa wa Baraza la Mawaziri uliokuwepo ulikuwa na lengo la kugawanya majukumu kwamba kila waziri afanye kazi katika eneo dogo, na baada ya kuona majukumu hayo yametekelezeka ipasavyo, sasa ameamua kupunguza idadi ya mawaziri. Rais alisema baada ya kupita miaka miwili ya serikali ya awamu ya nne walilazimika kufanya tathmini na baadaye kuona umuhimu wa kupunguza na kuunganisha baadhi ya wizara. Wizara pekee iliyoondolewa ni ya Siasa na Uhusiano wa Jamii, iliyokuwa ikiongozwa na Bw. Kingunge Ngomale-Mwiru na kwamba shughuli za wizara hiyo zitakuwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu. Aidha Wizara ya Mipango, Uchumi na Uwezeshaji na Fedha zimeunganishwa na kuwa moja wakati Tume ya Mipango itaundwa upya ili kiwe chombo kikuu cha serikali na kitakuwa chini ya Ofisi ya Rais. Wizara ya Mambo ya Ndani na ile ya Usalama wa Raia, nazo zimerudi kama awali na kuwa wizara moja. Wizara ya Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia na ile ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, alisema zinaunganishwa na kuwa wizara moja. Hata hivyo, alisema kutokana na ongezeko la shule za sekondari za kata, elimu ya sekondari na ya msingi zitasimamiwa na Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI). Kwa mujibu wa Rais Kikwete, masuala yote yanayohusisna na elimu, akimaanisha kuanzia ile ya awali, yatakuwa kwenye wizara moja. Aidha alisema, masuala yote yanayohusu Sayansi, Taknolojia kwa maana mawasiliano, posta, simu, teknolojia ya habari na mawasiliano, nazo zitakuwa kwenye wizara moja. Rais alisema, Kamati ya Usimamizi ya Pamoja ya kushughulikia masuala ya Muungano, yatakuwa chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais na kwamba ndiye atakayekuwa mwenyekiti wa vikao vya mazungumzo ya Muungano.
Kuhusu Idara ya Umwagiliaji iliyokuwa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika sasa shughuli hizo zitahamia wizara ya Maji, wakati uvuvi iliyokuwa Wizara ya Maliasili na Utalii, sasa shughuli zake zinahamishiwa Wizara ya Mifugo. Kwa upande wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, alisema Katibu Mkuu wa Wizara ya Sheria na Katiba ndiye alikuwa Naibu Mwanasheria Mkuu, lakini sasa Katibu Mkuu wa wizara hiyo atakuwa mtu tofauti ili abaki na jukumu la utawala.
SOURCE: Nipashe 13/02/2008

Monday, February 11, 2008

Baraza la Mawaziri

Leo tarehe 11/02/2008 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete anatarajiwa kutangaza Baraza lake jipya la Mawaziri. Baraza la mawaziri lilivunjwa kutokana na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania Ndg. Edward Lowasa kuachia ngazi kutokana na kuhushishwa na ufisadi wa Kampuni hewa ya Richmod.

Raisi wa Tanzania ameshamchagua Waziri Mkuu Mpya ambaye ni Ndg. Mizengo Pinda. Waziri Mkuu Mpya aliapishwa jumamosi tarehe 10/2/2008

Inatarajiwa na wananchi walio wengi kuwa Raisi atalipunguza baraza lake la mawaziri kutoka mawaziri 29 na manaibu mawaziri 31 na kuwa na baraza dogo zaidi.