Sunday, October 21, 2007


Lucky Dube born in August 3, 1964, died on October 18, 2007. He was killed by unknown people who are considered to be gangsters. I was shocked once I heard the death of Reggae composer the then Lucky Dube in South Africa . My favority music is reggae. For this case I lost very important friend of mine.
What worried me much is the killers killed Lucky Dube infront of his son and daughter. I don't believe if we will get some one to fill the gap left by Lucky Dube. I pray to God to rest Lucky Dube in a peace place.

Monday, October 8, 2007

HISTORY OF MY LIFE

Background information
My name is Emmanuel Patroba Mhache, a first born of Mr. and Mrs Patroba Joel Mhache and Trifosa Eliona Foya respectively. My beloved father is an Accountant Grade One by professional. While my mother is a house mother and engaging in farming activities. I was born in Manzese Uzuri, Kinondoni District, Dar es Salaam, Ocean Road Hospital in 24th December 1970s. My name has a meaning resembling this date, means "God With Us".
Educational Background
I got my education in different part of the country. Studied Primary Education which took me seven years at Moshi Rural, Kilimanjaro at Foyeni Primary School. I started standard one in 1979 and completed standard seven in 1985. Thereafter, I joined Natiro Secondary School for Form One in 1987 to Form Four in the year 1990. I completed my ordinary level education with flying colours.
With my good performance in Ordinary SecondarySchool I was selected to go for higher education studies. I joined Galanos High School for Form five and six studies in Tanga from 1991 to 1993. In July to December I joined the compulsory National Services (JKT) at Oljoro Camp for six months from July 1993 to December 1994.
From January to July 1995 I was doing business in Kimara, Dar es Salaam. I was supervising my fathers' shop located at Rombo, Kimara. Sometime I was co-shopkeeper and superviser.
Thereafter, in October 1995 I joined the University of Dar es Salaam for first degree programme. I pursued Bachelor of Arts Degree which I successfully accomplished in 1998 and awarded First Degree i.e. Bachelor of Arts Degree of the University of Dar es Salaam. After graduating I secured employment with PRIDE Tanzania Limited as Credit Officer.
I further joined University of Dar es Salaam for Master of Arts degree in Geography and Environmental Management which I accomplished successfully and awarded Master of Arts degree of the University of Dar es Salaam in 2004. I am now working with the Open University of Tanzania as an Assistant Lecurer in the Department of Geography. I am teaching geography. My roles are teaching, researching and doing consultations.

Monday, September 24, 2007

UMUHIMU WA KUWEKA MAZINGIRA YETU SAFI

Ni ukweli usiofichika kwamba mazingira yanapokuwa safi huvutia macho. Na ni kinga tosha ya magonjwa kwani wadudu kama mbu watakosa mahali pa kuzalia. usafi huanzia tunapoishi. Kusafi na kudeki nyumba zetu kila wakati. Kufagia mazingira kuzunguka nyumba zetu na kupanda maua na kuyatunza. Haya yote hufanya mazingira yetu kuwa na muonekano mzuri.
Cha kushangaza au sijui nisemeje ni kukuta mtu ni msafi awapo njiani au kazini, ukifanikiwa kufika anapoishi unaweza kushangaa, kwani hakuna tofauti na jalala la Tabata. Pia ofisini ni pasafi kiasi kwamba unaweza kuvua viatu na kuingia peku. Je ni kwanini huwa hivyo?

Friday, August 31, 2007

MAISHA NA KIPATO

Maisha ni mlima na ni kitendawili. Katika maisha kuna makundi mengi ya maisha kutokana na tafsiri ya mtu na vigezo alivyojiwekea. Kuna wale wenye maisha ya juu maisha ya kifahari. Kundi hili lina ishi kwenye nyumba nzuri, lina usafiri wa ghali na lina ulinzi wa mali zake. Wengi wa kundi hili wanaishi kwenye nyumba za serikali au wanalipiwa kodi na huduma nyingine kama maji, umeme n.k. na serikali au mashirika mbalimbali.
Pia kuna kundi la pili ambalo linaishi maisha ya kati, hili ni kundi ambalo chakula si tatizo kwao. ila halina kipato kinachowawezesha kuishi maisha ya juu. Kundi hili linaweza kuwa na nyumba bali huduma kama maji huw ani tatizo mara nyingine. Wachache wana nyumba zao.
Kundi la mwisho ni lile lenye maisha magumu. Kupata chakula au mlo mmoja kwa siku ni shida. kundi hili linaishi kwa kudra za mwenyezi Mungu. Kulala na njaa si tatizo kwao. Kwa upande wa mjini kundi hili huishi kwenye nyumba za kupanga na hasa kwenye yale maeneo ambayo huduma muhimu kama maji ni shida.
Je! Maisha si kitendawili?

Tuesday, August 28, 2007

CHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIA KIPO WAPI

Mimi ni mmoja wa Wahadhiri wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (Open University of Tanzania). Ni chuo kinachotoa elimu yake kwa njia ya masafa yaani Distance Education. Unapata elimu popote pale ulipo hapa Tanzania, haijalishi upo kijijini au mjini. Wengi wamejiunga na wamehitimu na kupata kazi nzuri kila pembe ya Tanzania na hata nje ya nchi.
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kipo wapi? Makao makuu ya chuo hiki yapo Tanzania, jijini Dar es Salaam katika wilaya ya Kinondoni. Ni chuo chenye mtandao nchi nzima. Kila mkoa una ofisi yake.
Ukitaka kujua zaidi kuhusu Chuo Kikuu Huria cha Tanzania soma kupitia www.openuniversity.ac.tz.
Karibu usome ukiwa unaendelea na majukumu yako.

Sunday, August 12, 2007

KITI-MOTO

Nguruwe ni mnyama anayefugwa. Hutembea kwa miguu minne. Mnyama huyu kwa watu ana fikra mbili. Moja kulingana na imani ya watu ni mnyama aliyekatazwa na MUNGU au na maandiko kuliwa kama kitoweo. Kwa upande wa pili ni chakula kizuri na nyama yake ni tamu sana.
Pamoja na fikra hizo, mnyama huyu hutoa faida zifuatazo kwa binadamu:
1. Nyama ijulikanayo na wengi kama "KITIMOTO"
2. Mbolea kwa ajili ya mazao
3. Kipato (income) kwa wafugaji wawauzapo hupata fedha pia wasafirishaji.
4. Ajira kwa wachinjaji na wauzaji wa jumla na rejareja
Week-end hii nilitembelea maeneo ya Mbezi Inn na kupata kinywaji bar moja iitwayo Green Park View. Bar hii ina sehemu ya kuuzia vinywaji kama beer, soda n.k. Pia wanatoa huduma ya chakula, chips, ndizi (za kukaanga na choma), nyama choma ya mbuzi, ngombe na kitimoto. Kitimoto hupikwa kutokana na matwaka ya mteja. Kwani kuna nyama ya Ku-Roast na kawaida iliyokaangwa tu. Na wengine huja kununua na kupeleka majumabni mwao.
Kwa utafiti wangu usio-rasmi "observation and participatory"niliona zaidi ya asilimia 70 ya wateja wanaoenda eneo hilo ni kupata "kitimoto" na wala sio kinywaji. Nilibahatika kuongea na mwenye mradi huo wa kitimoto na kunieleza kwamba biashara hiyo imemjengea heshima katika jamii. Kwani ameweza kujenga nyumba mbili zenye thamani kubwa, moja hapa mjini na nyingine Moshi Vijijini maeneo ya Kiboriloni. Pia anawasomesha watoto wake katika shule za msingi na secondary. Biashara hiyo pia imemjengea marafiki wengi kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na nje ya nchi. Mwisho biashara hii inampatia mlo wa kila siku bila tatiza lolote. Kwa ujumla maisha ni mazuri kwake.
Karibuni eneo hili muone hayo niliyoyaainisha hapo juu.
Asanteni kwa kusoma.

Friday, August 10, 2007

WIKIEND NA BURUDANI

Dear Wana Blog,
Ijumaa ni siku ya mwisho wa wiki kwa wale wafanyakazi. Ukitaka ujue ni ijumaa, wiki-endi hii tembelea maeneo ys sinza utaona mambo mengi na utakuwa umejifunza mengi kuhusu watu wanavyoishi maisha tofauti. Maisha ya hali ya juu, hali ya kati, ya kawaida na hali ya chini kabisa.
Karibuni.

Monday, August 6, 2007

MANZESE MPYA SEHEMU YA PILI

Kwa walio wengi wetu wanaweza wasiamini. Ila ni ukweli usiofichika kwamba kwa biashara, eneo la Manzese kumekucha. Ni aghalabu sana kuona eneo hili likiwa tupu bila watu. Eneo hili lipo bize wakati wote mchana hadi usiku. Wapo wanaotoka makazini, kwenye biashara zao, na wafanyabiashara wanaofanya biashara eneo hili la Manzese. Pia wapo wanaotoka kwenye starehe baada ya kazi ngumu za mchana.
Biashara kubwa iliyopo eneo hili ni ya KUSAGA na KUKOBOA NAFAKA, asilimia kubwa ikiwa ni mahindi. Unga ni chakula kikuu hasa hapa Dar es Salaam, kwa kiasi kikubwa unga huo unatoka eneo hili la Manzese. Je! Manzese si mahala pa kupaheshimu sasa? Muda wote wa siku masaa 24 mashine ya kusaga nafaka zinafanya kazi. Biashara/kazi hii imetoa ajira ya moja kwa moja kwa wananchi walio wengi, kwa waendesha mashine na wanaosafisha na kuchambua hizo nafaka kabla ya kusaga au kukoboa. Pia wafugaji wanapata pumba kwa ajili ya mifugo yao kama ng'ombe, mbuzi, nguruwe, kuku, n.k. Kilicho na faida hakikosi matatizo au lawama. Tatizo kubwa ni makelele yanayotokana na machine hizo pamoja na vumbi la nafaka.
Pia zipo biashara kubwa na ndogo ndogo kama maduka ya jumla, maduka ya watu binafsi ya vyakula na ujenzi. Pia zipo Bar, Groceries, maduka ya dawa, uuzaji wa vifaa vilivyotumika (used equipments), n.k.
Asanteni kwa kusoma.

Sunday, August 5, 2007

MANZESE MPYA

Manzese ni sehemu ambayo watu wengi wana mawazo kwamba si mahala pazuri pa kuishi. Siku hadi siku maeneo mengi ya Manzese yanaboreshwa ikiwemo Manzese Uzuri eneo ambalo nimeishi toka mwaka 1995 hadi sasa ninapoandika NEWS hii. Uboreshaji wa Manzese ni kutokana na juhudi za wana-Manzese, ufadhili wa Serikali ya Tanzania na Benki ya Dunia (World Bank).
Barabara inayopita eneo hilo imejengwa kwa kiwango cha lami. Barabara za mitaa ndio sasa zinawekwa kokoto ili ziweze kupitika kwa muda wote wa mwaka bila matatizo yoyote.

Kilichokuwa kilio cha wakazi wengi wa eneo hili la Manzese ni MAJI. Miundo mbinu ya maji ndio sasa inakamilika. Na baada ya muda mfupi tatizo la maji katika eneo hili litakuwa ni historia.
Eneo hili la Manzeze halipo nyuma katika maendeleo ya elimu. Shule za msingi zipo za kutosha. wanafunzi wamalizapo elimu ya mzingi lengo lao ni kwenda sekondari. Wana-Manzese nikiwa mmoja wao tuliliona hilo na kuoa michango ya fedha, nguvu zetu n.k., kwa sasa eneo hili lina shule moja ya secondari inayoitwa Mazese Secondary School.
Baadae nitaelezea maendeleo katika sector ya biashara, nyumba za ibaada n.k. See you next time.
Karibuni Manzese mjionee maendeleo kwa ujumla.
Mhache

Thursday, August 2, 2007

MAZINGIRA NA MAISHA

Ni ukweli usiofichika kwamba mazingira mazuri yanavutia watu kuishi. Lakini kuna watu wasioona umuhimu huo. Ukitembelea maeneo ya Manzese utashangaa kwani ni kawaida kuamka asubuhi na kukuta furushi la taka mlangoni mwako au kuzunguka nyumba yako. Unajiuiza hawa watu wana akili timamu au la. Nimejaribu kuwauliza na watu wachache, majibu yao yalikuwa ya kukatisha tamaa. Wengine walisema hizo taka niliziweka mimi, wengine wakasema hawaoni ni kwa nini watupe hapo wakati kuna sehemu ya kutupa hizo taka.

Kila la heri wana-blogu

HABARI WANABLOGU NA JUMUIYA YA WANABLOGU TANZANIA.

Ndugu wanablogu nimejiunga na dunia ya blogu,natumai wote tutashirikiana kuinua na kupanza sauti katika jamii.

Karibuni wote.