Friday, July 25, 2008

Ongezeka la watu na matumizi ya misitu

Misitu ni rasilimali muhimu sana kwa matumizi ya binadamu. Kutokana na misitu tunapata kuni, mbao, majengo, dawa, chakula cha binadamu kama matunda na malisho ya wanyama. Misitu pia hutoa faida nyingine kama kivuli, kuzuia mmomonyoko wa udongo, mabadiliko ya hali ya hewa na mengine.

Tatizo ni kutokuwa na matumizi endelevu ya misitu, watumiaji wa misitu waelimishwe matumizi bora ya misitu. Wananchi wanakata miti bila kutoa muda kwa misitu hiyo kuota. Hii inatokana na ongezeko la watu kutoendana na uwezo wa misitu kutoa faida hizo. Pia watumiaji wa misitu hawapandi miti baada ya kuvuna.